Na Mapuli
Misalaba, Shinyanga
Halmashauri ya Manispaa
ya Shinyanga leo imekabidhi vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu
mbalimbali msaada ambao ulitolewa na
mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu
anayeshughulikia kazi vijana na ajira Patrobas Katambi
Jumla ya watu 42 wenye
ulemavu wamekabidhiwa vifaa hivyo katika
ofisi za shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu SHIVYAWATA Mkoa wa
Shinyanga
Akikabidhi vifaa hivyo
kwa wenye ulemavu wa viungo na wasioona Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya
Shinyanga Elizabeth Mweyo ametoa
Baiskeli 6 zenye magurudumu matatu za watu wenye ulemavu, fimbo nyeupe 20
kwa ajili ya wasioona pamoja na magongo 16 ya kutembelea, huku akiwasisitiza
walengwa kutobadili matumizi yaliyokusudiwa katika vifaa hivyo
“Kuna baadhi huwa mnapewa Baiskeli mnaenda kuziuza hamjapewa
kwahiyo sababu, mmepewa kwa sababu ya kuwasaidia ziwarahisishie kufanya
majukumu yenu ya kila siku kwahiyo msiende kuziuza tutawafuatilia kwa sababu
orodha yenu tunayo tutawafuatilia kujua hivyo vifaa mnavitumia, mnazo,
zinafanya kazi au mmeshaziuza”
Baada ya kupokea msaada
huo baadhi ya watu wenye ulemavu waliopatiwa
vifaa hivyo wamemshukuru mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu
kazi vijana na ajira Patrobas Katambi na serikali kwa ujumla
Kwa upande wake
mwenyekiti wa chama cha walemavu Mkoa wa Shinyanga Bwana Mohamed Ally amewataka
wale wote waliobahatika kupata msaada huo kuvitunza vifaa hivyo saidizi ili viweze
kudumu
Naye mwenyekiti wa shirikisho
la vyama vya watu wenye ulemavu SHIVYAWATA
mkoa wa Shinyanga Richard Mpongo
amewaomba watu wenye ulemavu
kushirikiana na vyama vyao vyote pamoja na kujitokeza watu wenye ulemavu ambao
hawatambuliki kwenye vyama
0 Comments