WANANACHI WAJITOKEZA KUCHANJA BAADA YA WATOA HUDUMA KUWAFUATA

 

Mmoja wa wananchi wilayani Kasulu akipata chanjo baada ya watoa huduma kuwafikia

Na Deogratius Nsokolo

Wananchi katika kata za nyachenda na asante nyerere katika halmashauri ya wilaya ya kasulu mkoani kigoma, wamesema hatua ya wataalam wa afya kutembea katika vitongoji na vijiji kuhamasisha na kutoa chanjo ya ugonjwa wa uviko 19 inasaidia watu wengi na hasa wazee wasio na uwezo wa kutembea umbali mrefu kupata huduma ya chanjo ya corona.

Wamesema hatua ya wahudumu wa afya kuwafuata wananchi imeondoa hofu na kufanya idadi kubwa ya watu kujitokeza kupata elimu na kuamua kuchanja ambapo wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na kuhakikisha chanjo zinakuwepo katika maeneo yote ya kutolea huduma vijijini.

Mtoa huduma akitoa elimu kuhusu chanjo ya Uvico 19 kwa baadhi ya wananchi wilayani Kasulu mkoani Kigoma

Kwa upande wake mratibu wa chanjo katika halmashauri ya wilaya ya kasulu elia  thomas  amesema watoa huduma katika halmashauri hiyo wameweza kuvifikia vijiji vyote ikiwa ni pamoja na maeneo muhimu kama masoko na minada ili kutoa huduma ambapo amewahimiza wananchi kuendelea kujitokeza kupokea chanjo ya uviko 19 ili kujikinga na ugonjwa huo.

Post a Comment

0 Comments