ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 63 ZIMEPOKELEWA NA TASAF MKOANI KIGOMA

 


Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Zaidi ya Shilingi Bilioni 63 Zimepokelewa Katika Mfuko wa Maendeleo ya Jamii wa kunusuru kaya Masikini  Mkoani Kigoma, ambapo zaidi ya Shilingi  Bilioni 53 kati ya hizo tayari zimewafikia walengwa hadi kufikia Mwezi March 2021.

Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Kigoma Msafiri Nzunuri, alieleza hayo wakati akisoma Tarifaa ya Sekta ya  Maendeleo ya Jamii, katika Kikao kazi kilichowakutanisha Viongozi Mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya ndani  Christopher Kadio.

Wakati huo huo baadhi ya Wazee kutoka Baraza la Wazee Mkoani hapa , waliiomba Serikali kuongeza Juhudi za kuweka Mazingira wezeshi zaidi kwa kundi hilo, ili wasiendelee kuwa tegemezi kwa Watoto wao.


Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dk John Jingu, alilithibitishia kundi la Wazee hapa nchini kuwa Serikali itaendelea kuboresha Mazingira rafiki kwao, huku Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya ndani Christopher Kadio akisema Wazee wanamchango Mkubwa Kwa Maendeleo Ya Taifa. 

 

Post a Comment

0 Comments