Na Mwajabu Hoza ,
Kigoma
Mkoa
wa Kigoma umezindua Kampeni ya kukabiliana na vitendo vya ukatili wa
kijinsia itakayo jumuisha wadau mbalimbali watakao iwezesha jamii na mamlaka
husika kushirikiana kwa pamoja kutokomeza vitendo hivyo.
Kampeni hiyo yenye kauli mbiu isemayo “Twende pamoja ukatili wa kijinsia Kigoma
sasa basi” itajumuisha Mkundi kadhaa ikiwemo wanahabari, viongozi wa dini,
wasanii na wazee watakaoiwezesha jamii kupata elimu sahihi juu ya vitendo vya
ukatili.
Kigoma imetajwa kuwa miongoni mwa mikoa inayotekeleza vitendo vya ukatili wa
kijinsia na ukatili wa kingono kwa makundi ya wanawake na watoto na matukio
mengi yameshindwa kufanyiwa kazi ipasavyo kutokana na matukio hayo
kufanyika ndani ya familia na kuishia kumalizwa kifamilia.
Afisa
ustawi wa jamii mkoa wa Kigoma Elisha Nyamala amesema kwa mwaka kumekuwa na
matukio ya ukatili kati ya 200 hadi 300 yanaripotiwa kutoka katika wilaya zote
za mkoa wa Kigoma na matukio 1014 yameripotiwa na kati ya hayo 34 yametolewa
hukumu wengine wamehukumiwa kifungo cha maisha na wengine wamehukumuwa
kifo.
Mkurugenzi idara ya maendeleo ya jamii kutoka wizara ya afya maendeleo ya jamii
jinsia wazee na watoto Mwajuma Magwiza amesema elimu ni miongoni mwa sababu ya
kutokomeza ukatili wa kijinsia ambapo kampeni hiyo itakuwa jumuishi kwa
kwa kushirikisha wadau wa maendeleo , mashirika , asasi , na jamii na lengo ni
kila mmoja kwa nafasi yake kuhakikisha wanatumia fursa aliyonayo kutoa elimu.
Ukiachilia mbali madhara ya kisaikolojia na kimwili kwa mtu aliyefanyiwa
vitendo vya ukatili,uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa unatajwa kuathirika kwa
kupoteza nguvu kazi.
Mkuu wa mkoa Kigoma Thobias Andengenye amesema serikali imekuwa ikiwekeza zaidi
kwenye ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ya elimu, Afya, barabara na
reli na lengo ni jamii kutumia miundombinu hiyo kwa maslahi yao na Taifa hivyo
ikiwa jamii moja inamaumivu yanayotokana na vitendo vya ukatili
inakuwa vigumu kutumia vyema miundombinu hiyo na kujikuta Taifa linakuwa
na jamii yenye vinyongo na chuki.
0 Comments