TSH. BILIONI 2.3 KUTATUA KERO YA MAJI WILAYANI BUHIGWE

 


Na Emmanuel Matinde, Kigoma

Zaidi ya wananchi elfu kumi wa Kijiji cha Mwayaya Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, wanatarajia kupata huduma ya maji safi na salama baada ya mradi wa maji wa chanzo cha mto Kivuruga unaojengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 2.3 chini ya ufadhili wa Shirika la Enabel kukamilika.

Hayo yalielezwa na Eng. Respicius Kahamba, Mhandisi wa Maji kutoka Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA Wilaya ya Buhigwe, ambaye amesema kwa sasa ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia zaidi ya 90%.

Alisema mradi huo Pamoja na miradi mingine inayotekelezwa katika Wilaya ya Buhigwe  yote kwa Pamoja ikigharimu zaidi ya Shilingi Bilioni tisa, itaongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.

Wakati hayo yakiendelea Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Tanganyika, ilibainisha mikakati ya kukabiliana na tishio la uharibifu wa chanzo cha mradi wa maji wa Kijiji cha Mwayaya ili kuhakikisha unakuwa endelevu.

 Wakati huo huo mradi wa maji wa Kijiji cha Mnanila katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe ambao unajengwa kwa fedha za UVIKO 19 Shilingi Milioni 400 umeanza kutoa maji.

Wilaya ya Buhigwe ina jumla ya vijiji 44 ambapo ambapo kwa sasa asilimia 72 ya vijiji hivyo ndiyo hupata maji safi na salama.

 

Post a Comment

0 Comments