WANANCHI WASHAURIWA KUWA NA DESTURI YA KUPIGA MAZOEZI


Na Mwandishi Wetu, Kigoma.

Wananchi Mkoani Kigoma wameshauriwa kuwa na desturi ya kufanya mazoezi na kupima afya zao mara kwa mara ili kuweza kuondokana na magonjwa nyemelezi.

Wito huo ulitolewa na Afisa Mahusiano kutoka Benki ya CRDB Makao Makuu Bw. Timoth Fasha wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ufanyaji wa Mazoezi uliopewa jina la Wellness Day ambayo imefanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika.

Bw.Timoth alisema kuwa wafanyakazi wamekuwa hawapati muda wa kufanya mazoezi kutokana na majukumu walionayo ofisini na hivyo Benki ya CRDB wameamua kutenga siku ya kuwakutanisha wafanyakazi wao ili kufanya mazoezi na kuimarisha afya zao.

Naye Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa siku ya Wellness day, Bw. Ngassa Maxmiliani akimwakilisha Mkuu wa Wilaya Kigoma Bi. Esther Mahawe alisema  hakuna shughuli yoyote ambayo inaweza kufanyika bila kuwa na afya njema hivyo mazoezi muhimu kwa kila mwanadamu.

Akizungumza kwa niaba ya Wafanyakazi wa matawi yote ya Benki ya CRDB Mkoani Kigoma, Meneja wa CRDB tawi la Kigoma Bw. Arrison Andrew alisema wamefurahishwa na mtakakati wa banki yao kuwa na program hiyo kwani kutofanya mazoezi muda mwingi unaweza kukumbwa na magonjwa.

Uzinduzi wa Kampeni hiyo ya Wellness Day umeenda sambamba na zoezi kupima afya zao kwa wafanyakazi na wananchi waliojitokeza uwanjani hapo.

 


Post a Comment

0 Comments