VIJANA WAMETAKIWA KUTOYACHUKULIA POA MAFUNZO YA MGAMBO

 

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na vijana waliohitimu mafunzo ya mafunzo ya jeshi la akiba (mgambo) Manispaa ya Kigoma ujiji October 27, 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe  akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya mafunzo ya jeshi la akiba (mgambo) Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Vijana waliohitimu mafunzo ya mafunzo ya jeshi la akiba (mgambo) Manispaa ya Kigoma ujiji October 27, 2022 wakimsikiliza mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe.


Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Vijana na watu wa rika zote nchini wametakiwa kutoyachukulia poa mafunzo ya jeshi la akiba (mgambo) badala yake wajitokeze kupata mafunzo hayo kwa kuwa yana faida nyingi lakini kubwa zaidi ni kijana kuwa mzalendo kwa taifa lake.

Mara nyingi mtazamo wa jamii umekuwa kwamba askari wa jeshi la akiba, au kama wanavyojulikana kwa jina la Mgambo, ni watu wasumbufu na waonevu kwa raia kutokana na kutumiwa na mamlaka za ngazi ya halmashauri katika shughuli mbalimbali, hasa pale wanapoonekana kwenye uvunjaji wa vibanda vya biashara ya wamachinga.

Hata hivyo sivyo ilivyo, kama Chatta Emmanuel Kitanga na Hellen Mlondo ambao ni wahitimu wa mafunzo ya mgambo walivyoeleza kuwa mafunzo ya mgambo yanawafanya vijana kuwa wakakamavu na pia kuwa na utimamu wa akili.

“Hatupewi mafunzo na vibaka ila tumepewa mafunzo na Askali wa jeshi la wananchi hivyo ni mafunzo halali kabisa ambayo pia ni mlango wa fulsa kwetu” wamesema vijana hao.

Aidha askari wa jeshi la akiba wamekuwa na faida nyingi kwa halmashauri; ni kutokana na umuhimu wao Mshauri wa Mgambo Wilaya ya Kigoma Suleiman Mgeni Kassim, ameutaka uongozi wa halmashauri kuwathamini.

“Tunaomba ofisi hasa halmashauri kuwaongezea kipato vijana wa mgambo ili waweze kukabiliana na maisha ili wasiingiwe na tama, ila pia kwa vijana mliohitimu hii leo hakikisheni mnaendeleza mazoezi” amesema.

Akifunga mafunzo ya jeshi la akiba, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Eshter Mahawe,  amewataka wahitimu wa mafunzo kutoyatumia mafunzo hayo kufanya ukatili majumbani mwao au katika jamii wanayoishi.

“Msibadirishe muelekeo, msitumie uzoefu mlioupata kwenda kuwatishia wazazi au ndugu zenu huko nyumbani, kazi yenu ni kulinda raia na kuwa tayari muda wowote mtakapohitajika katika kulinda mipaka ya nchi yetu” amesema Mahawe.

Mafunzo ya jeshi la akiba ni sera ya ulinzi wa Taifa, na hutolewa kila mwaka na kila wilaya kote nchini.

 

 

Post a Comment

0 Comments