Na Mwajabu Hoza , Kigoma
UMOJA wa wamiliki na wasifirishaji wa maboti Mkoani Kigoma UWAMAKI wameomba serikali kuwa na mkakati wa kikabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola kwa kuwa na vifaa vya kisasa vya kupima ugonjwa huo ambavyo vitasaidia kubaini wagonjwa wenye dalili na kuepusha watu wengi kukaa karantini wakisubiri hatma yao kwa muda mrefu.
Mweyekiti wa umoja huo Kashindi Adam amesema eneo la Kibiriza ambapo wageni kutoka nchi za Congo DRC na Burundi huingia na kutoka nchini, vipimo vinavyotumika ni vile vya kupima joto la mwili pekee na kudai inaweza kusababisha watu wengi ambao hawana maambukizi hayo kuweka karantini.
“Tunaiomba serikali iweze kutupatia vifaa vya kisasa ambavyo vitatumiwa na
wahudumu wa afya waliopo katika eneo letu la kibirizi kuwapima wasafiri
wanaoingia na kutoka ili kama ikibainika mtu ana ugonjwa huo serikali iweze
kuchukua hatua za haraka” amesema
Mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma Dokta Jesca
Lebba amesema idara ya afya imeweka mikakati yote ya kuhakikisha wageni
wanaongia nchini wanafanyiwa vipimo na wale wenye dalili kutengwa sehemu
maalumu ambazo tayari zimeandaliwa.
Amesema hatua zingine zilizochukuliwa ni pamoja na kuwaagiza wahudumu ngazi ya jamii kutoa elimu juu ya dalili, jinsi ya kujikinga na wapi watu wanaweza patiwa msaada pindi wanapokuwa na mtu mwenye maambukizi.
“Idara ya afya tumejitahidi kuweka tahadhari katika maeneo yote ya mipakani ikiwemo katika maeneo ya bandari zote, kiwanja cha ndege na maeneo ambayo yanaingilika kwa urahisi na jamii kuingia na kutoka, pia tumeweka tahadhari kwa kuwa na wataalamu pamoja na vifaa vya kufanyia vipimo lengo ni kuhakikisha mkoa unakuwa salama” amesema
Mambukizi ya Ugonjwa wa Ebola hadi sasa
umeripotiwa nchini Uganda mwezi Septemba mwaka huu.
0 Comments