Na Mwandishi Wetu, Kigoma
Wakulima kutoka
wilaya mbalimbali za mkoa wa Kigoma, wamelazimika kuweka kambi kwa mawakala wa
kuuza mbolea ya ruzuku ya serikali, kutokana na kuendelee kusubiri mbolea hiyo
kwa zaidi ya wiki moja kwa mawakala wanaosambaza bila mafanikio, huku
changamoto ikitajwa kukosekana kwa stika licha ya mbolea hio kufungiwa kwenye
maghala ya kuuzia.
Wakizungumza na
Kituo hiki Wakulima hao wamesema wanalazimika kutumia ghalama kubwa za kulala
katika nyumba za wageni ili kusubiria mbolea huku changamoto hio ikikwamisha
shughuli za kilimo.
Akieleza sababu
za kutogawa mbolea kwa wakati, mmoja wa wakala wa kusambaza mbolea ya ruzuku
Kutoka kampuni ya ETG Sebastian Raurent amesema changamoto ya sitika ndio
imekwamisha ugawaji wa mbolea hiyo, na kwamba juhudi za kuweka sitika
zinafanyiwa kazi.
Aidha Afisa
kilimo, mifugo na uvuvi manispaa ya Kigoma Ujiji Evance Mdee alikanusha
changamoto ya ukosefu wa mbolea kuwepo kwa sasa na kuzitaka kampuni
zinazosimamia zoezi la ugawaji kulifanikisha kwa wakati.
0 Comments