WAZIRI MKUU AKUTANA NA WADAU WA ZAO LA CHIKICHI MKOANI KIGOMA

Na Mwandishi Wetu, Kigoma
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiongoza kikao kazi kilichomkutanisha na wadau wa Kilimo cha zao la chikichi mkoani Kigoma.

Awali akifungua kikao hicho, Waziri Mkuu amesema lengo la kukutana na wadau hao ni kufanya Tathimini ya Mafanikio yaliyofikiwa katika kuibua, kuendeleza na kuboresha kilimo cha zao la chikichi katika mkoa.

Kikao kazi hicho kinafanyika katika Ukumbi wa NSSF Manispaa ya Kigoma-Ujiji na kuwakutanisha Wakuu wa Wilaya, wakurugenzi watendaji wa Halmashauri, wazalishaji wa mbegu za chikichi, wamiliki wa viwanda vidogo vya kuchakata zao hilo pamoja na wakulima wakubwa na wadogo wa chikichi mkoani hapa.

Post a Comment

0 Comments