SERIKALI YA MANISPAA KIGOMA UJIJI YAANZA KAMPENI YA USAFI ZIWA TANGANYIKA


Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Serikali ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Saalam wameanza kampeni ya  usafi wa mazingira kwenye mialo na fukwe za ziwa Tanganyika

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Mhadhiri msaidizi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Saalam Bahati Bayoma amesema wamefanya kampeni hiyo kwa sababu  hadi kufikia mwishoni mwa Mwaka 2022  takwimu zinaonyesha kuwa  wastani  wa tani milioni 8 za taka za plastiki zinazozalishwa duniani zinaingia kwenye vyanzo vya maji.

Naye Afisa Usafi na Mazingira Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi. Petronia Gwakila amesema kampeni hiyo inamanufaa kwani itafanya mazingira kuwa masafi, huku akiwataka wavuvi na wananchi kutilia maanani suala la usafi wa mazingira kwenye maeneo wanayoishi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Bangwe Said Betese akiwa na baadhi na viongozi wa wavuvi katika Mwalo wa Katonga wamesema mazingira yanapokuwa masafi yanasaidia kutokuwepo kwa mlipuko wa magonjwa hasa kipindupindu.

Post a Comment

0 Comments