Kuhusu Ugonjwa maambukizi ya ngozi ya juu ya gololi la jicho (Viral Conjuctivitis) maarufu kama red eyes 👀👀
Zingatia haya ujikinge:
➡️Usiguse guse macho; maambukizi hutoka kwenye viganja vya mikono kuja kwenye macho
➡️ Nawa mikono kwa maji tiririka na sabuni
➡️Wakuu vitakasa mikono muhimu sana kipindi kama hiki
➡️Usichangie vipodozi na vitu vingine unavyotumia kama vile wanja, tishu, nguo au dawa za macho nk
➡️ Usishike mikono watu hovyo, iwapo umeshika takasa mikono
Pia zingatia yafuatayo:
➡️Kutokutumia dawa zisizo rasmi na ambazo hazijaandikwa na daktari.
➡️Usitumie dawa za macho anazotumia mgonjwa mwingine au alizoandikiwa yeye awali alipokuwa na tatizo la jicho ili kuepuka madhara.
0 Comments