Na Emmanuel Matinde, Kigoma.
Taasisi ya
Moyo ya Jakaya Kikwete JKCI kupitia huduma ya tiba mkoba iliyoanzishwa na Rais
Samia Suluhu Hassan imeweka kambi ya siku tatu mkoani Kigoma kwa ajili kutoa
huduma ya upimaji wa magonjwa ya moyo kwa watoto na watu wazima pamoja na kutoa
elimu ya jinsi ya kujikinga na magonjwa hayo.
Akitoa
taarifa ya kambi hiyo Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa Watoto kutoka Taasisi
ya Moyo ya Jakaya Kikwete Dr. Eva Wakuganda, amesema tatizo la magonjwa ya moyo
ni kubwa hapa nchini ambapo tangu kuanza kwa mfuko wa tiba mkoba chini ya Rais
Samia asilimia 40% ya watu elfu 11,254 waliofikiwa wamebainika kuwa na magonjwa
hayo.
Kwa upande
wake, Mratibu wa Huduma za Kitabibu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma
Maweni Dr. Bonipace Kilangi amesema kulingana na takwimu za hospitali za robo
ya tatu ya mwaka magonjwa ya moyo pamoja na shinikizo la damu ni namba mbili baada
ya magonjwa upasuaji.
Baadhi ya
wananchi waliofika kunufaika na huduma hiyo walikuwa na haya ya kusema.
Zaidi ya watu
mia tatu wanatarajiwa kuonwa na madaktari bingwa katika kambi hiyo mkoani
Kigoma.
0 Comments